Breaking News

Friday, October 20, 2017

ZLSC YAFANYA KONGAMANO LA SIKU YA ADHABU YA KIFO DUNIANI

Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar, kiliungana na Mataifa mengine duniani kufanya  kongamano la siku ya kupinga Adhabu ya Kifo Duniani ambayo kikawaida hufanyika kila ifikapo tarehe 10.10 kila mwaka.

Kwa mwaka 2017 maadhimisho hayo yalifanyika  kijiji cha Uvivini, kisiwani Tumbatu  kwa Unguja na Ukumbi wa Jeshi la Polisi Chake Chake  kwa Pemba.

Lengo la kongamano hilo ni kukutana na Wadau mbali mbali kwa ajili ya kuelezea hali halisi ya utekelezaji wa hukumu ya kifo na kukusanya maoni.
Kauli mbiu ya mwaka huu ni "UMASIKINI ISIWE SABABU YA KUHUKUMIWA KIFO"



Washiriki wa Kongamano la siku ya kimataifa ya kupinga Adhabu ya Kifo wakiwa safarini kuelekea  kijiji cha Uvivini kisiwani Tumbatu, kwa ajili ya maadhimisho 

Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar  Prof. Chris Maina Peter ,akitoa ufafanuzi  wa  adhabu ya Kifo kwa  wananchi wa kijiji cha Uvivini kisiwani Tumbatu, katika kongamano la siku ya kimataifa  la kupinga Adhabu ya Kifo Duniani

Mratibu   wa Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar,  Ofisi ya Pemba Bi. Fatma Khamis Hemed, akiwakaribisha washiriki wa Kongamano la Siku ya kimataifa la kupinga adhabu ya kifo lilifanyika Ukumbi wa Jeshi la Polisi Chake Chake Pemba   

Washiriki wa Kongamano  wakisiliza kwa makini mada  inayotolewa, katika Kongamano lilifanyika Ukumbi wa Jeshi la Polisi Chake Chake Pemba

No comments:

Post a Comment

Designed By Published. Moonga Stephen