Breaking News

Wednesday, September 13, 2017

MAFUNZO KWA MASHEHA NA DIWANI WA WILAYA YA KATI

Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar kimeandaa mafunzo kwa Masheha wa Wilaya ya Kati  yaliyofanyika  katika Ukumbi wa ZLSC Kijangwani mjini Unguja, tarehe 13 Septemba 2017
Lengo la mafunzo hayo ni kuwatambulisha Wasaidizi wa Sheria kwa Masheha na kuwataka  Masheha,  kuwatumia Wasaidizi wa Sheria na   kushirikiana nao katika kutetea  na kuzilinda haki za binadamu.

Kaimu Mkurugenzi wa Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar,  Bi.Saida Amour Abdallah akifungua mafunzo  kwa Masheha  wa Wilaya ya Kati Unguja, yaliyofanyika tarehe 13 Septemba 2017  Kijangwani mjini Unguja

Afisa Mipango wa ZLSC Bi Moza Kawambwa Nzole akiwasilisha mada ya dhana ya Wasaidizi wa Sheria  kwa washiriki wa mafunzo  kwa  Masheha wa Wilaya ya kati
Read more ...

Tuesday, September 12, 2017

MAFUNZO YA WAZAZI JUU YA MALEZI SALAMA NA MASHIRIKIANO YA BABA

Kituo cha  Huduma za Sheria Zanzibar, kimefanya mafunzo kwa wazazi juu ya malezi salama na mashirikiano ya baba, yaliyofanyika katika ukumbi wa ZLSC Kijangwani mjini Unguja.
Mafunzo hayo ya siku tatu yalikuwa na lengo la kuwashirikisha baba katika malezi ya watoto (Male Engagement on Positive Parenting) kutokana na baba wengi kuwaachia jukumu  akina mama na kusahau wajibu wao.
Kupitia mafunzo hayo wanaume walipata elimu ya kutosha juu ya namna ya kushirikiana na wanawake  katika malezi ili kuhakikisha watoto wanapata malezi bora na salama.
Mafunzo hayo ya siku tatu yalianza tarehe 10 Septemba 2017 na kumalizika tarehe 12 Septemba 2017.

Wazazi  wakiwa katika mafunzo ya malezi salama na mashirikiano ya baba, yaliyofanyika katika Ukumbi wa ZLSC Kijangwani mjini Unguja, tarehe 12 Septemba 2017
Read more ...
Designed By Published. Moonga Stephen