Breaking News

Wednesday, August 9, 2017

MAFUNZO YA KUWATAMBULISHA WASAIDIZI WA SHERIA KWA WATUMISHI WA IDARA MAALUM (VIKOSI) SMZ


Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar kimefanya mafunzo ya kuwatambulisha Wasaidizi wa Sheria kwa Watumishi wa Idara maalum (Vikosi) vya SMZ. Mafunzo hayo yamefanyika katika ukumbi wa ZLSC kijangwani Mjini Unguja tarehe  09 Agosti 2017 kwa lengo la kutoa uelewa wa sheria kwa  watumishi hao.

Akizungumza katika mafunzo hayo, mratibu  ambae ni Afisa Mipango wa Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar Bi Moza   Nzole aliwataka watumishi hao kufuata haki na sheria katika utendaji wao ili kuwafanya raia wawe na imani juu ya vikosi hivyo.


Washiriki wakiwa katika mafunzo ya kuwatambulisha Wasaidizi wa Sheria kwa watumishi wa Idara Maalu ( vikosi) SMZ yaliyofanyika  katika ukumbi wa ZLSC Kijangwani mjini Unguja tarehe 09 Agosti 2017 

No comments:

Post a Comment

Designed By Published. Moonga Stephen