Breaking News

Wednesday, December 6, 2017

KITUO CHA HUDUMA ZA SHERIA ZANZIBAR CHAADHIMISHA MIAKA 25

Tarehe 2 Disemba 2017, Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar kiliadhimisha miaka 25  tokea kuanzishwa  kwake   sambamba  na kumbukizi ya  muasisi wa Kituo Marehemu Profesa Haroub Othman, iliyofanyika ukumbi wa  Baraza la Wawakilishi  la zamani, Kikwajuni  mjini Unguja.

Mgeni Rasmi katika maadhimisho hayo alikuwa ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Issa Haji  Ussi (Gavu)  ambaye alikipongeza Kituo kwa kuweza kufikisha miaka 25.

Maadhimisho hayo pia yalifuatiwa na uzinduzi wa Kitabu cha Miaka 25 ya Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar  pamoja na kutolewa zawadi kwa waanzilishi wa Kituo na Wajumbe wa Bodi waliotangulia.
Baadhi ya washiriki wa Maadhimisho ya miaka 25 ya Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar na kumbukizi ya Muasisi wa Kituo Marehemu Prof. Haroub Othman

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Issa Haji  Ussi (Gavu) akizindua kitabu cha Miaka 25 ya Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar, katika maadhimisho yaliyofanyika Ukumbi wa Baraza la Wawakilishi la zamani Kikwajuni mjini Unguja,  (kati kati)  Kaimu Mkurugenzi wa  Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar,  akifuatiwa na Afisa Mipango Bi. Moza Kawambwa Nzole

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Issa Haji Ussi (Gavu) akionesha kitabu cha Miaka 25 ya Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar, baada ya kukizindua (kulia) ni Mwenyekiti wa Bodi wa  Kituo Prof. Chris Maina Peter

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Issa Haji  Ussi (Gavu)  akimkabidhi zawadi muanzilishi na  aliyekuwa Mjumbe wa Bodi  wa Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar,  Bi. Fatma Maghimbi

No comments:

Post a Comment

Designed By Published. Moonga Stephen