Breaking News

Saturday, March 11, 2017

MAFUNZO YA HAKI ZA BINAADAMU KWA WAANDISHI WA HABARI YALIYOFANYIKA KATIKA UKUMBI WA MIKUTANO WA ZLSC KIJANGWANI ZANZIBAR TAREHE 11\03\2017


 Baadhi ya Waandishi wa habari wakiwa katika ukumbi wa
ZLSC  kusubiria mafunzo ya Haki Za Binaadamu..

Afisa Mipango  Thabit Abdullah kutoka Kituo cha Huduma za
Sheria Zanzibar (ZLSC)   akiwasilisha mada ya Haki za
Binaadamu na nafasi ya Waandishi wa habari kwa jamii. 
Mwanasheria   Rashid Abdallah akiwasilisha mada ya
Madhara ya Rushwa katika usimamizi wa Haki za Binaadamu.


Mshauri wa vyombo vya Habari  Salim Said Salim akiwasilisha
 mada  kuhusu kanuni, miiko na maadili ya Waandishi wa
Habari Kitaifa na Kimataifa.

Waandishi wa Habari wakisikiliza kwa makini mada
zinazowasilishwa katika mafunzo hayo.
Read more ...

Wednesday, March 8, 2017

MAAZIMISHO YA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI YALIYOFANYIKA KATIKA UKUMBI WA KITUO CHA HUDUMA ZA SHERIA ZANZIBAR KIJANGWANI TAREHE 7/03/2017

WAZIRI WA ELIMU NA MAFUNZO YA AMALI ZANZIBAR,  RIZIKI PEMBE JUMA AKITOA HOTUBA YA MAADHIMISHO YA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI.

Siku ya wanawake duniani huadhimishwa kimataifa  kila mwaka ifikapo Terehe 8 Machi, lengo kuu ni kumuendeleza mwanamke kiuchumi, kijamii, na  kisiasa ili kumpa fursa ya  kuwa na maendeleleo endelevu.

 Kwa kuzinagatia hilo Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar kwa kushirikiana na Asasi tofauti zisizo za kiserikali  ambazo ni ZAFELA, TAMWA, ZGC, SOS, Action Aid na Save New Generation, wamekuwa mstari wa mbele katika kuadhimisha siku ya Wanawake duniani ambapo Mgeni Rasmi katika hafla hiyo ni Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Riziki Pembe Juma, na kauli mbiu  ya mwaka huu ilikua"Imarisha fursa za ajira kwa kumuezesha mwanamke kiuchumi" .

Siku ya wanawake duniani ilianza mwanzoni mwa  mwaka 1900's kwa kupitia wanawake wafanyakazi wa sekta ya viwanda nchini Marekani kuandamana kwa kupiga vita udhalilishaji na ukandamizwaji uliokuwa ukitokea katika maeneo ya kazi yakiwemo mazingira magumu na hatari,,ukosefu wa huduma za jamii pamoja na unyanyasaji,  .

Kuna mikakati mbali mbali inachukuliwa  ili kumuinua mwanamke katika nyanja zote za kiuchumi, kisiasa na kijamii, ikiwemo kuundwa kwa tume mfano TAMWA. Kuwepo kwa dawati la jinsia, wanawake na watoto, pamoja na kumuinua kielimu kwa kuwawekea skuli maalum mfano Benbella Girls Secondary School ili kuwakuza wanawake kifikra kwa lengo la kupata usawa wa kijinsia kati ya mwanamke na mwanamme.


Jumla ya washiriki 50 walihudhuria maadhimisho hayo wakiwemo Wanaharakati wa Wa Haki za Binaadamu na masuala ya Kijinsia yaliyofanyika tarehe 07/03/2017 katika ukumbi wa Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar.









Read more ...
Designed By Published. Moonga Stephen