Breaking News

Tuesday, October 24, 2017

KITUO CHA HUDUMA ZA SHERIA ZANZIBAR KIMEFANYA MAFUNZO YA WASAIDIZI WA SHERIA KWA JUMUIYA YA ZAWOPA(Zanzibar Women Paralegal)


Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar kimeandaa  mafunzo ya siku mbili kwa  Jumuia ya Wasaidizi wa Sheria Wanawake  (ZAWOPA).  Mada mbali mbali  ziliwasilishwa ambazo ni Ndoa na Talaka, Malezi Bora, Matunzo na Ukaazi wa Mtoto kwa Mujibu wa Sheria ya Mtoto, Dhana ya Ugatuzi, Sheria ya Mahakama ya Ardhi pamoja na Rushwa na Changamoto katika Ardhi.

Mafunzo hayo ya siku mbili yameanza leo tarehe 24 na kumaliza kesho tarehe 25 Oktoba 2017 kwa lengo la kutoa uelewa juu masuala mbali mbali ya kijamii na kuendelea kuwajengea uwezo Wasaidizi wa Sheria waliokwisha hitimu mafunzo yao.


Kaimu Mkurugenzi wa Kituo cha Huduma Zanibar
 Bi. Saida Amour Abdalla akifafanua aina za talaka
                                 


Wasaidizi wa Sheria wakifanya kazi za vikundi 



Msaidizi wa Sheria akiwasilisha  kazi ya kikundi






No comments:

Post a Comment

Designed By Published. Moonga Stephen