Breaking News

Sunday, December 10, 2017

ZLSC YAADHIMISHA SIKU YA HAKI ZA BINADAMU DUNIANI

Kamishna wa Tume ya Haki za Binadamu  Bw. Mohammed  Khamis akiwasilisha mada ya Dhana ya Haki za Binadamu katika Maadhisho ya Siku ya Haki za Binadamu Duniani, yaliyofanyika katika ukumbi wa Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar, Kijangwani mjini Unguja.  Kushoto ni Kamanda Msaidizi wa Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi Bw. Haji Abdalla Haji na kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa ZLSC Bi Saida Amour Abdalla

Washiriki wakisiliza mada ya Haki za Binadamu katika maadhimisho ya Siku ya Haki za Binadamu Duniani yaliyofanyika katika ukumbi wa ZLSC Kijangwani mjini Unguja

Mshiriki akichangia mada

Kamanda Msaidizi wa Polisi Mkoa wa Mjini Mgharibi Bw. Haji Abdalla Haji  ( aliyekaa katikati) akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa Bodi  wa ZLSC, Wafanyakazi, na Wadau wengine baada ya  maadhimisho ya Siku ya Haki za Binadamu Duniani yaliyofanyika Kijangwani mjini Unguja. Kulia ni Kamishna wa Tume ya Haki za Binadamu Bw. Mohammed Khamis na  kushoto ni  Mjumbe wa Bodi wa ZLSC Bi. Salma Saadati  

Read more ...

Wednesday, December 6, 2017

KITUO CHA HUDUMA ZA SHERIA ZANZIBAR CHAADHIMISHA MIAKA 25

Tarehe 2 Disemba 2017, Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar kiliadhimisha miaka 25  tokea kuanzishwa  kwake   sambamba  na kumbukizi ya  muasisi wa Kituo Marehemu Profesa Haroub Othman, iliyofanyika ukumbi wa  Baraza la Wawakilishi  la zamani, Kikwajuni  mjini Unguja.

Mgeni Rasmi katika maadhimisho hayo alikuwa ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Issa Haji  Ussi (Gavu)  ambaye alikipongeza Kituo kwa kuweza kufikisha miaka 25.

Maadhimisho hayo pia yalifuatiwa na uzinduzi wa Kitabu cha Miaka 25 ya Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar  pamoja na kutolewa zawadi kwa waanzilishi wa Kituo na Wajumbe wa Bodi waliotangulia.
Baadhi ya washiriki wa Maadhimisho ya miaka 25 ya Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar na kumbukizi ya Muasisi wa Kituo Marehemu Prof. Haroub Othman

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Issa Haji  Ussi (Gavu) akizindua kitabu cha Miaka 25 ya Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar, katika maadhimisho yaliyofanyika Ukumbi wa Baraza la Wawakilishi la zamani Kikwajuni mjini Unguja,  (kati kati)  Kaimu Mkurugenzi wa  Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar,  akifuatiwa na Afisa Mipango Bi. Moza Kawambwa Nzole

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Issa Haji Ussi (Gavu) akionesha kitabu cha Miaka 25 ya Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar, baada ya kukizindua (kulia) ni Mwenyekiti wa Bodi wa  Kituo Prof. Chris Maina Peter

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Issa Haji  Ussi (Gavu)  akimkabidhi zawadi muanzilishi na  aliyekuwa Mjumbe wa Bodi  wa Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar,  Bi. Fatma Maghimbi
Read more ...

Sunday, December 3, 2017

KUMBUKIZI YA MAREHEHEMU PROFESA HAROUB OTHMAN

Wanafunzi wakimuombea dua Muasisi wa Kituo cha  Huduma za Sheria
Zanzibar,
 Marehemu Prof. Haroub Othman

Wanafunzi wakisoma dua  

Wafanyakazi wa Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar wakijumuika na
wanafunzi katika kumuombea dua muasisi  wao. Mungu ailaze
roho ya Marehemu  mahala pema peponi. AMIN 

Read more ...

Thursday, November 23, 2017

MAFUNZO YA KUWAKUMBUSHIA MRADI WA WATOTO WANAOKINZANA NA SHERIA KWA MAAFISA WA CHUO CHA MAFUNZO

Baadhi ya Maafisa Polisi  wa  Chuo cha Mafunzo, wakiwa katika mafunzo ya kukumbushwa juu ya Mradi wa Watoto Wanaokinzana na Sheria, yaliyoandaliwa   na Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar

Read more ...

Friday, November 3, 2017

BALOZI WA UFARANSA AMETEMBELEA ZLSC

Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar kimetembelewa na Balozi wa Ufaransa Bi Malika BERAK kwa lengo la kutaka kujua shughuli mbali mbali zinazofanywa na Kituo.

Kaimu Mkurugenzi wa Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar Bi Saida Amour Abdalla, akimfafanulia Balozi wa Ufaransa Bi. Malika BERAK kazi za Kituo

Read more ...

Thursday, October 26, 2017

MKUTANO WA MWAKA KWA WADAU WA KITUO (ZLSC)

Kaimu Mkurugenzi Wa Kituo Cha Huduma Za Sheria Zanziabar
Bi Saida Amour akiwasilisha taarifa ya kazi za Kituo kwa mwaka
2017,katika Mkutano hou.




Mmoja wa washidau wa Kituo Bi Suzani Kunambi akichangia
 mada  baada ya kupokea taarifa ya kazi zilizofanywa na
Kituo kwa mwaka
2017.



Read more ...

Tuesday, October 24, 2017

KITUO CHA HUDUMA ZA SHERIA ZANZIBAR KIMEFANYA MAFUNZO YA WASAIDIZI WA SHERIA KWA JUMUIYA YA ZAWOPA(Zanzibar Women Paralegal)


Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar kimeandaa  mafunzo ya siku mbili kwa  Jumuia ya Wasaidizi wa Sheria Wanawake  (ZAWOPA).  Mada mbali mbali  ziliwasilishwa ambazo ni Ndoa na Talaka, Malezi Bora, Matunzo na Ukaazi wa Mtoto kwa Mujibu wa Sheria ya Mtoto, Dhana ya Ugatuzi, Sheria ya Mahakama ya Ardhi pamoja na Rushwa na Changamoto katika Ardhi.

Mafunzo hayo ya siku mbili yameanza leo tarehe 24 na kumaliza kesho tarehe 25 Oktoba 2017 kwa lengo la kutoa uelewa juu masuala mbali mbali ya kijamii na kuendelea kuwajengea uwezo Wasaidizi wa Sheria waliokwisha hitimu mafunzo yao.


Kaimu Mkurugenzi wa Kituo cha Huduma Zanibar
 Bi. Saida Amour Abdalla akifafanua aina za talaka
                                 


Wasaidizi wa Sheria wakifanya kazi za vikundi 



Msaidizi wa Sheria akiwasilisha  kazi ya kikundi






Read more ...

Monday, October 23, 2017

KITUO CHA HUDUMA ZA SHERIA ZANZIBAR KILIFANYA MKUTANO WA KUANDAA MPANGO KAZI

Picha ya pamoja kati ya wajumbe wa bodi, wafanyakazi, washauri na wadau wengine wa ZLSC  katika kuandaa mpango kazi wa Kituo wa mwaka 2018/2022, uliofanyika  Z-Ocean Hoteli,  Bububu Meli nane kuanzia tarehe 14 hadi 16 Oktoba 2017  

Baadhi ya washiriki wa Mkutano wa kuandaa mpango kazi wa Kituo wakimsikiliza kwa makini mshauri

Read more ...

ZLSC YAFANYA TATHMINI YA MAFUNZO YA UTAYARISHAJI KATIBA NA SHERIA KWA VIJANA WA MABARAZA YA VIJANA YALIYOFANYIKA TAREHE 9 OKTOBA 2017

Afisa Ufuatiliaji na Tathmini Bw. Mohammed Kh. Mohammed akitoa ufafanuzi juu ya tathmini, katika  mkutano wa tathmini ya mafunzo ya elimu ya uraia kwa Vijana wa Mabaraza ya Vijana uliofanyika, ZLSC Kijangwani tarehe 09 Oktoba 2017

Mshiriki  katika mkutano wa tathmini  akielezea kwa washiriki wenziwe  mafanikio aliyoyapata baada ya mafunzo ya elimu ya uraia aliyopatiwa na Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar 

Read more ...

KITUO CHA HUDUMA ZA SHERIA ZANZIBAR KIMEFANYA KONGAMANO LA KUPINGA ADHABU YA KIFO DUNIANI


Read more ...

KITUO CHA HUDUMA ZA SHERIA ZANZIBAR, KILIFANYA MAFUNZO YA HAKI ZA BINADAMU KWA WADAU TAREHE 7 NA 8 OKTOBA 2017 -KIJANGWANI

Washiriki wa mafunzo ya Haki za Binadamu, wakifanya kazi za vikundi  

Baadhi ya washiriki wa mafunzo ya Haki za Binadamu  wakifuatilia kwa makini mada ya   dhana ya udhalilishaji iliyowasilishwa na  Afisa Mipango Bi Jamila Masoud ( hayupo pichani)

Read more ...

MAADHIMISHO YA SIKU YA MTOTO WA KIKE

Mgeni Rasmi, Mkurugenzi Idara ya Elimu Sekondari Bi Asya Iddi Hassan ( katikati) akifuatilia igizo kuhusu udhalilishaji ,  lililogizwa na THESODE ,(hawapo pichani),  katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa kike yaliyofanyika ZLSC Kijangwani tarehe 11 Oktoba 2017 wa pili kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa ZLSC Bi. Saida Amour Abdalla akifuatiwa na  Mratibu Bi. Jamila Masoud,  wengine ni  Dokta Fatma wa Hospitali ya Mnazi Mmoja  na Bi. Sabra Msellem kutoka DPP 

Wanafunzi wa skuli mbali mbali za Unguja wakisikiliza  mada ya Ukatili wa Kijinsia na Athari za Mimba za Utotoni, iliyowasilishwa  na Dokta Fatma kutoka hospitali ya Mnazi Mmoja 

Read more ...

Friday, October 20, 2017

KITUO CHA HUDUMA ZA SHERIA ZANZIBAR KILIFANYA ZIARA YA KUTEMBELEA KLABU ZA ELIMU YA URAIA KATIKA SKULI ZA MIKOA MITATU YA UNGUJA

Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar kikiwasili katika moja ya  skuli ilizotembelea ambayo ni skuli ya sekondari Jumbi kwa lengo la kutembelea  klabu ya wanafunzi skulini hapo. 

Afisa Mipango wa Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar Bw. Ali Haji Hassan akiwa na watoto waliopelekwa skuli  na walimu  wa skuli ya Jumbi baada ya watoto hao kukosa  haki ya  elimu bila sababu za msingi na umri ukiwa umesonga ,  Haya ni matunda ya ZLSC baada ya kuwapatia  elimu ya uraia walimu  wa skuli mbali mbali 

Wafanyakazi wa Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar Bw Mohammed Kh. Mohammed wa (kwanza kushoto) na Bw. Ali Haji Hassan (wa kwanza kulia)   wakiwa na Afisa elimu kutoka Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali  Bw. Daudi Suhuba  ( alievaa suti ya kijijvu jivu) pamoja na  walimu wa skuli ya Paje,wakizungumzia maendeleo ya klabu  walipofika skulini hapo kutembelea klabu hiyo

Baadhi ya wanafunzi wa Skuli ya Ndijani waliojiunga na Klabu ya Elimu ya uraia wakimsikiliza Afisa Mipango  Bw. Ali Haji Hassan ( hayupo pichani) 

Wanafunzi wa  klabu ya skuli ya Paje wakifanya igizo la Udhalilishaji
Wanafunzi wa Skuli ya Kombeni wakiimba wimbo wa  kutokomeza udhalilishaji

Read more ...

ZLSC YAFANYA KONGAMANO LA SIKU YA ADHABU YA KIFO DUNIANI

Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar, kiliungana na Mataifa mengine duniani kufanya  kongamano la siku ya kupinga Adhabu ya Kifo Duniani ambayo kikawaida hufanyika kila ifikapo tarehe 10.10 kila mwaka.

Kwa mwaka 2017 maadhimisho hayo yalifanyika  kijiji cha Uvivini, kisiwani Tumbatu  kwa Unguja na Ukumbi wa Jeshi la Polisi Chake Chake  kwa Pemba.

Lengo la kongamano hilo ni kukutana na Wadau mbali mbali kwa ajili ya kuelezea hali halisi ya utekelezaji wa hukumu ya kifo na kukusanya maoni.
Kauli mbiu ya mwaka huu ni "UMASIKINI ISIWE SABABU YA KUHUKUMIWA KIFO"



Washiriki wa Kongamano la siku ya kimataifa ya kupinga Adhabu ya Kifo wakiwa safarini kuelekea  kijiji cha Uvivini kisiwani Tumbatu, kwa ajili ya maadhimisho 

Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar  Prof. Chris Maina Peter ,akitoa ufafanuzi  wa  adhabu ya Kifo kwa  wananchi wa kijiji cha Uvivini kisiwani Tumbatu, katika kongamano la siku ya kimataifa  la kupinga Adhabu ya Kifo Duniani

Mratibu   wa Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar,  Ofisi ya Pemba Bi. Fatma Khamis Hemed, akiwakaribisha washiriki wa Kongamano la Siku ya kimataifa la kupinga adhabu ya kifo lilifanyika Ukumbi wa Jeshi la Polisi Chake Chake Pemba   

Washiriki wa Kongamano  wakisiliza kwa makini mada  inayotolewa, katika Kongamano lilifanyika Ukumbi wa Jeshi la Polisi Chake Chake Pemba

Read more ...

Thursday, October 5, 2017

MAFUNZO YA HAKI ZA BINADAMU KWA WATU WALIOATHIRIKA NA UTUMIAJI WA DAWA ZA KULEVYA YALIYOFANYIKA TAREHE 05 OKTOBA 2017

Afisa Mipango wa Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar, Bw. Thabit Abdulla Juma akitoa mada ya Haki za Binadamu kwa watu walioathirika na utumiaji wa dawa za kulevya, katika mafunzo yaliyofanyika  ZLSC Kijangwani , mjini -Unguja, tarehe 05 Oktoba 2017

Read more ...

ZIARA YA WANAFUNZI WA SKULI YA SEKONDARI KWARARA KWA KITUO CHA HUDUMA ZA SHERIA ZANZIBAR

Mwanafunzi wa skuli ya Sekondari Kwarara akielezea  mafunzo aliyoyapata baada ya kuja kituoni katika ziara ya kukitembelea Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar, kilichopo Kijangwani mjini Unguja,  ziara hiyo ilifanyika tarehe 03 Oktoba 2017

Read more ...

Wednesday, September 13, 2017

MAFUNZO KWA MASHEHA NA DIWANI WA WILAYA YA KATI

Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar kimeandaa mafunzo kwa Masheha wa Wilaya ya Kati  yaliyofanyika  katika Ukumbi wa ZLSC Kijangwani mjini Unguja, tarehe 13 Septemba 2017
Lengo la mafunzo hayo ni kuwatambulisha Wasaidizi wa Sheria kwa Masheha na kuwataka  Masheha,  kuwatumia Wasaidizi wa Sheria na   kushirikiana nao katika kutetea  na kuzilinda haki za binadamu.

Kaimu Mkurugenzi wa Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar,  Bi.Saida Amour Abdallah akifungua mafunzo  kwa Masheha  wa Wilaya ya Kati Unguja, yaliyofanyika tarehe 13 Septemba 2017  Kijangwani mjini Unguja

Afisa Mipango wa ZLSC Bi Moza Kawambwa Nzole akiwasilisha mada ya dhana ya Wasaidizi wa Sheria  kwa washiriki wa mafunzo  kwa  Masheha wa Wilaya ya kati
Read more ...

Tuesday, September 12, 2017

MAFUNZO YA WAZAZI JUU YA MALEZI SALAMA NA MASHIRIKIANO YA BABA

Kituo cha  Huduma za Sheria Zanzibar, kimefanya mafunzo kwa wazazi juu ya malezi salama na mashirikiano ya baba, yaliyofanyika katika ukumbi wa ZLSC Kijangwani mjini Unguja.
Mafunzo hayo ya siku tatu yalikuwa na lengo la kuwashirikisha baba katika malezi ya watoto (Male Engagement on Positive Parenting) kutokana na baba wengi kuwaachia jukumu  akina mama na kusahau wajibu wao.
Kupitia mafunzo hayo wanaume walipata elimu ya kutosha juu ya namna ya kushirikiana na wanawake  katika malezi ili kuhakikisha watoto wanapata malezi bora na salama.
Mafunzo hayo ya siku tatu yalianza tarehe 10 Septemba 2017 na kumalizika tarehe 12 Septemba 2017.

Wazazi  wakiwa katika mafunzo ya malezi salama na mashirikiano ya baba, yaliyofanyika katika Ukumbi wa ZLSC Kijangwani mjini Unguja, tarehe 12 Septemba 2017
Read more ...

Monday, August 14, 2017

ZLSC YAENDELEA KUTOA MAFUNZO KWA VIJANA WA BARAZA LA VIJANA KWA MKOA WA KUSINI UNGUJA JUU YA ELIMU YA URAIA

Kaimu Mkurugenzi wa Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar,  Bi Saida Amour Abdalla, akifungua mafunzo  kwa Vijana wa Baraza la Vijana kwa Mkoa wa Kusini Unguja, yaliyofanyika katika ukumbi wa ZLSC,  Kijangwani mjini Unguja, tarehe 14 Agosti, 2017 

Read more ...

Friday, August 11, 2017

TATHMINI YA KUJADILI MPANGOKAZI WA KITUO WA MWAKA 2013/2017


 Wadhamini, Wafanya tathmini, Wajumbe wa Bodi wa Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar, wafanyakazi na wadau wengine, wakiwa katika kikao cha tathmin ya kujadili mpango kazi wa Kituo,  uliofanyika katika ukumbi wa Umoja wa Watu Wenye Ulemavu Zanzibar (UWZ) mjini Unguja tarehe  11 August 2017
Read more ...

Wednesday, August 9, 2017

ZLSC YATOA MAFUNZO KWA VIJANA WA BARAZA LA VIJANA KWA MKOA WA KASKAZINI UNGUJA JUU YA ELIMU YA URAIA YALIYOFANYIKA

KITUO cha Huduma za Sheria Zanzibar chatoa mafunzo ya elimu ya uraia kwa vijana wa  baraza la vijana kwa Mkoa wa Kaskazini,  Unguja.
Mfunzo hayo yalifanyika  katika ukumbi wa ZLSC Kijangwani tarehe 09 Agosti 2017   kwa lengo la kutoa uelewa wa elimu ya uraia kwa vijana.


Washiriki wakiwa katika mafunzo ya elimu ya uraia kwa vijana wa Baraza la vijana  kwa Mkoa wa Kaskazini Unguja  yaliyofanyika katika ukumbi wa ZLSC Kijangwani tarehe 09 Agosti 2017

Read more ...

MAFUNZO YA KUWATAMBULISHA WASAIDIZI WA SHERIA KWA WATUMISHI WA IDARA MAALUM (VIKOSI) SMZ


Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar kimefanya mafunzo ya kuwatambulisha Wasaidizi wa Sheria kwa Watumishi wa Idara maalum (Vikosi) vya SMZ. Mafunzo hayo yamefanyika katika ukumbi wa ZLSC kijangwani Mjini Unguja tarehe  09 Agosti 2017 kwa lengo la kutoa uelewa wa sheria kwa  watumishi hao.

Akizungumza katika mafunzo hayo, mratibu  ambae ni Afisa Mipango wa Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar Bi Moza   Nzole aliwataka watumishi hao kufuata haki na sheria katika utendaji wao ili kuwafanya raia wawe na imani juu ya vikosi hivyo.


Washiriki wakiwa katika mafunzo ya kuwatambulisha Wasaidizi wa Sheria kwa watumishi wa Idara Maalu ( vikosi) SMZ yaliyofanyika  katika ukumbi wa ZLSC Kijangwani mjini Unguja tarehe 09 Agosti 2017 

Read more ...

Monday, August 7, 2017

MKUTANO WA NUSU MWAKA KWA WASAIDIZI WA SHERIA


Mratibu wa Mafunzo ya wasaidizi wa sheria  Bi  Moza Nzole akiwa katika Mkutano wa nusu mwaka kwa wasaidizi wa sheria kujadili matarajio, mwelekeo mapungufu pamoja na changamoto za mradi wa wasaidizi wa sheria Zanzibar uliofanyika tarehe 07 August 2017 katika ukumbi wa ZLSC Kijangwani mijini Unguja
Read more ...

MAFUNZO YA USHIRIKISHWAJI WANANCHI KATIKA UTAYARISHAJI WA KATIBA NA SHERIA


KITUO  cha Huduma za Sheria Zanzibar kimetoa
mafunzo kwa viongozi wa dini na watendaji wa
Serikali za Mitaa kuhusu Ushirikishwaji wananchi
katika utayarishaji Katiba na Sheria.

Mafunzo hayo yalifanyika Tarehe  07 Agosti 2017
katika ukumbi wa Kituo  Kijangwani mjini Unguja
kwa lengo la kuwajengea uwezo wa namna Sheria
na Katiba zinavotayarishwa


Mratibu wa mafunzo ambae ni Afisa Mipango wa
Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar Bw Ali Haji
Hassan akiwasilisha mada ya namna ya ushirikishwaji
wananchi katika utayarishaji Katiba na Sheria  katika
mafunzo yaliyofanyika  ZLSC Kijangwani
yaliyowajumuisha viongozi wa dini na watendaji wa
serikali za mitaa
Read more ...
Designed By Published. Moonga Stephen