Breaking News

Tuesday, September 12, 2017

MAFUNZO YA WAZAZI JUU YA MALEZI SALAMA NA MASHIRIKIANO YA BABA

Kituo cha  Huduma za Sheria Zanzibar, kimefanya mafunzo kwa wazazi juu ya malezi salama na mashirikiano ya baba, yaliyofanyika katika ukumbi wa ZLSC Kijangwani mjini Unguja.
Mafunzo hayo ya siku tatu yalikuwa na lengo la kuwashirikisha baba katika malezi ya watoto (Male Engagement on Positive Parenting) kutokana na baba wengi kuwaachia jukumu  akina mama na kusahau wajibu wao.
Kupitia mafunzo hayo wanaume walipata elimu ya kutosha juu ya namna ya kushirikiana na wanawake  katika malezi ili kuhakikisha watoto wanapata malezi bora na salama.
Mafunzo hayo ya siku tatu yalianza tarehe 10 Septemba 2017 na kumalizika tarehe 12 Septemba 2017.

Wazazi  wakiwa katika mafunzo ya malezi salama na mashirikiano ya baba, yaliyofanyika katika Ukumbi wa ZLSC Kijangwani mjini Unguja, tarehe 12 Septemba 2017

No comments:

Post a Comment

Designed By Published. Moonga Stephen