Breaking News

Wednesday, February 21, 2018

KITABU CHA ZANZIBAR YEAR BOOK OF LAW VOLUME 6 CHAZINDULIWA






Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mh. Dk. Ali Mohamed Shein,akionesha  kitabu  cha Zanzibar Yearbook of Law Volume 6, 2016 baada ya kukizindua , katika  Maadhimisho ya Siku ya Sheria Zanzibar, yaliyofanyika katika Viwanja vya Baraza la Wawakilishi la zamani  Kikwajuni,  tarehe 12 Februari 2018. Kulia Jaji Mkuu wa Zanzibar  Mhe. Omar Othman Makungu   na kushoto ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la  Mapinduzi Mh. Issa Haji Gavu  


Rais wa Zanzibar na Mwenye Kiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein  amekizindua Kitabu cha Sheria cha mwaka Juzuu ya 6 ( Zanzibar Yearbook of Law (ZYBL), Volume 6) 2016, katika maadhimisho ya Siku ya Sheria yaliyofanyika  katika ukumbi wa Baraza la Wawakilishi la Zamani  Kikwajuni mjini Unguja.

Uwepo wa  ZYBL unatokana na kazi kubwa inayofanywa na Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar kwa kushirikiana na wadau wengine kwa lengo la kutoa uelewa juu ya masuala mbali mbali ya kisheria ya ndani na nje ya nchi. Hivyo ni vyema jamii kukitumia  kitabu hiki.







1 comment:

Designed By Published. Moonga Stephen